Mwengine ajitosa uwenyekiti ACT.

Mwanachama mwengine wa ACT wazalendo amechukua fomu ya Kugombea Uwenyekiti wa Taifa chama hicho  huku akiahidi kuongoza chama katika misingi bora katika umoja na mshikamano. Mwanachama huyo ambaye ni  Hamad Masoud Hamad aliyaeleza hayo mara badaa ya kuomba nafasi hiyo na kukabidhiwa fomu huko katika Ofisi ya chama hicho iliyopo Mtaa wa vuga Mjini Zanzibar